HOJA NEWS BLOG

TTCL KUUNGANISHA WILAYA ZOTE KWANYE MKONGO WA TAIFA.

HOJA NEWS BLOG Add Comment

 Na Prisca Libaga ,Arusha.

Mkurugenzi Ufundi wa Shirika la mawasiliano Nchini TTCL mhandisi Cecil  Francis ,kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa TTCL ,amesema wilaya 33 kati ya 139 ambazo hazijaunganishwa kwenye mkongo wa taifa zitaunganishwa mwaka huu na wakandarasi wanaendelea na kazi hiyo.

Ameyasema hayo Septemba 18 alipokuwa akizungumza na Vyombo vya habari kwenye kongamano la siku mbili la Wadau wa huduma za mtandao wa mawasiliano kwenye hoteli ya Gran Melia Jijini Arusha .

Amesema kuwa TTCL inafanya kazi ya kuhakikisha nchi inaongea kwa kuunganisha mkoa kwa mkoa ,Wilaya kwa Wilaya ambapo tayari wilaya 106 zimeshaunganishwa kwenye mkongo wa taifa.

Amesema kuwa mkongo huo wa taifa wa mawasiliano unaojengwa unapita kila mahali ukiwa na ubora kwa lengo la kutoa huduma bora kwa wananchina ndio kiungo kikuu cha Mawasiliano ambao umeunganishwa na mkongo wa bahari ambayo ndio inatupa Internet.

Mhandisi Francis amesema Shirika hilo lina dhamana kubwa ya kutoa huduma bora za mawasiliano kupitia mkongo wa taifa  ambao ulianza kutekeleza mwaka 2013.


Amesema kuwa wameunda mkongo huo na nchi jirani za Kenya, Uganda ,Rwanda, Burundi ,Zambia, Malawi na kuna maunganusho yanayoenda kwenye mpaka na Msumbijina sasa wanaanza kushughulikia maunganusho na nchi ya DRC Congo, kupitia ziwa Tanganyika hadi mji wa Kalemii Nchini DRC.


Ameongeza kuwa pia TTCL inashugulikia maunganisho  kwenda kwenye kituo  kilichopo baharini hadi Mombasa Nchini Kenya.


Amesema TTCL inaendelea kutoa mchango wa mawasiliano kuhakikisha mkongo unaojengwa inakuwa na ubora wa hali ya juu kwa lengo la kufikisha huduma  kwa Wananchi na kupunguza gharama.


Mhandisi, Francis,amesema nchi yetu ni kiunganishi kikuu cha Mawasiliano kwenye ukanda wetu wa nchi za EAC na SADC.


Mwisho.

AIRTEL KUBORESHA HUDUMA YA MAWASILIANO YA SIMU NCHINI.

HOJA NEWS BLOG Add Comment

 Na Prisca Libaga.

Mkurugenzi wa biashara Kampuni ya simu za mkononi, Airtel ,Joseph Muhere, amesema mwaka Jana kampuni hiyo imefunga mtambo mpya Submarinecable ambao ni mkubwa na una uwezo mkubwa wa kupokea na kutumia data kwa kiwango kikubwa ,uwekezaji huo umefanywa kwa ajili ya Watanzania na nchi jirani ambazo zinahitaji mawasiliano kwa njia ya mtandao.

Amesema kuwa kampuni hiyo mwaka huu 2024 inaendelea kufangua huduma  zake za mawasiliano katika miji na Vijiji ambapo kwa mjini kuwezesha kupata huduma ya 3G,4G,5G na Kampuni inaendelea na Uwekezaji na upanuzi wa mtandao maeneo ya Vijiji ili kuwezesha kupata huduma ya 3G 4G na 5G.

Muhere, ameyasema hayo Septemba 18  alipokuwa akizungumza na Vyombo vya habari kwenye kongamano la siku mbili la wadau wa mawasiliano  linalofanyika hoteli ya Gran Melia,Jijini Arusha .

Amesema kuwa lengo la Mkutano huo wa 8 ni kuwaleta Wadau wote pamoja katika teknolojia, ambapo kampuni hiyo inaendelea kuvifikia Vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na huduma hiyo ambapo sasa wanajenga huduma ya 5G kwa ajili ya wateja Ujenzi ambao unaenda sambamba na kuhakikisha gharama zinakuwa nafuu.

Mkutano huo wa Connect2Connect Summit umewakutanisha wadau wote wa mawasiliano nchini ikiwemo Airtel Tanzania chini ya kauli mbiu ya ‘Meaningful Connectivity’


Airtel wataonyesha namna gani Mkongo wa Chini ya Bahari wa Airtel 2 Africa utakavyochangia katika maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha mawasiliano kote nchini pamoja na namna ambavyo mkongo huo utasaidia kuiweka Tanzania kama kinara wa kidigitali katika ukanda wa Afrika Mashariki.



Mwisho.

DCEA YAFANYA UTEKETEZAJI WA DAWA ZA KULEVYA AINA YA MIRUNGI JIJINI ARUSHA

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Na Prisca Libaga Arusha

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini kwa niaba ya Kamishna Jenerali tarehe 13.09.2024 imeteketeza kwa mujibu wa sheria vielelezo vya dawa za kulevya aina ya mirungi kilogramu 23.74 zilizokamatwa katika operesheni zilizotekelezwa hivi karibuni. Uteketezaji wa vielelezo hivyo ulifanyika katika dampo la Murieti jijini Arusha. 

Zoezi hilo limeshuhudiwa na wawakilishi kutoka Mahakama ya Wilaya Arusha, Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Arusha, Ofisi ya Mkemia Mkuu Arusha kulingana na Matakwa ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. 








Mwisho.

WATUMISHI WA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA MATATANI TUHUMA ZA RUSHWA KWENYE UTALII.

HOJA NEWS BLOG Add Comment

 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoa wa Arusha kuanza uchunguzi dhidi ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Injinia Juma Hamsini na baadhi ya wasaidizi wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za rushwa na ubadhirifu wa fedha za walipa kodi.

Akizungumza na wadau wa utalii Mkoani Arusha leo Jumamosi Mei 18, 2024, Mhe. Paul Christian Makonda amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bw. Missaile Mussa kuwasimamisha kazi watumishi wote waliotajwa kuhusika na tuhuma hizo ili kupisha uchunguzi.



Mhe. Mkuu wa Mkoa amechukua hatua hizo baada ya Mwenyekiti wa waongoza watalii mkoa wa Arusha Wilbard John Chambulo kudai kuwa   baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wamekuwa wakitengeneza nyaraka bandia pamoja na kuchepusha baadhi ya makusanyo ya kodi zinazotokana na sekta ya Utalii.

Chambulo amemuambia Mkuu wa Mkoa kwamba Watumishi hao wamekuwa na makampuni hewa ya utalii pamoja na kuwa na namba tofauti za ulipaji wa kodi na usajili hewa wa makampuni yenye kufanana na makampuni halisi ya utalii yalipo ndani ya Jiji la Arusha.


Mara baada ya malalamiko hayo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amesema serikali yake inawajibikaji kuwa mlezi wa wafanyabiashara na wawekezaji wa mkoa wa Arusha na hivyo kamwe hatovumilia mtendaji yeyote anayekuwa sababu ya kukua kwa vitendo vya rushwa na kuua biashara zilizopo mkoani Arusha.


Aidha Mhe. Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku kwa Halmashauri zilizopo mkoani Arusha kutumia Polisi kwenda kudai kodi kwa wafanyabiashara na kuagiza zitumike teknolojia zaidi kwenye kukumbusha na kudai madai mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Arusha.


Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa Paul Christian Makonda amelazimika kuahirisha kikao kazi hicho na kuagiza kupangwa kwa tarehe nyingine chini ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha ili kupata muda mzuri wa kujadiliana na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazokwamisha ukuaji na ustawi wa sekta ya Utalii mkoani Arusha.

SOMALIA RASIMI MWANACHAMA MPYA WA NANE EAC

HOJA NEWS BLOG Add Comment

KATIBU MKUU EAC ASEMA WANANCHI NCHI WANACHAMA WAFIKIA MILIONI 350,SOKO LA PAMOJA AJIRA KUPANUKA

Nchi ya Somalia imejiunga Rasmi kuwa mwanachama wa nane wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika makao Makuu ya EAC Jijini Arusha na kuelezwa kuwa itasaidia suala Zima la msukumo wa changamoto za ajira kwa Nchi wanachama pamoja na kupanua soko la pamoja .

Aidha Kujiunga kwa Somalia ni kutokana na kikao cha Wakuu wa nchi kilichoketi  desemba  25 mwaka Jana jijini Arusha,kukubali Nchi hiyo kujiunga na jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akiongea na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Dkt.Peter Mathuki katika sherehe fupi ya kupandisha bendera na kupokea hati za unachama wa Somalia makao makuu ya EAC Jijini Arusha amesema soka la Jumuiya limepanua wigo na kuwa na watu takribani milioni 350 kwa Sasa na hivyo kuiwezesha jumuiya hiyo kujipanua kibiashara.

Aidha alisema kiwango cha ukuaji wa pato la EAC limeongezeka kutoka Dolla bilioni 2.5 Hadi Dola bilioni 3 na kuongeza soko la ajira kuondoa changamoto za ukosefu wa ajira kwa nchi wanachama na ongezeko la bidhaa kwa kuwa na watu milioni 350 kwa sasa.

Akiongelea suala la usalama Dkt.Mathuki amesema kuwa kuongezeka kwa soka hilo la watu wanaofikia milioni 350 kutaondoa changamoto za upungufu wa ajira na kupelekea wananchi kuchangamkia uzalishaji wa bidhaa na kuuza katika soko la pamoja.

"Hii ni Moja ya kuondoa changamoto za ajira na kurudisha Hali ya usalama katika mataifa ya Jumuiya ikiwa soko la Jumuiya kwa Sasa Lina watu takribani milioni 350 uzalishaji wa bidhaa utaondoa upungufu na kuzalisha ajira hivyo kuwepo kwa usalama katika nchi zetu"

Kwa Upande wake Waziri wa Habari wa Somalia Daud Aweso amesema wanayofuraha Kubwa kukamilisha safari ndef⁰mu ya miaka 12 na safari hiyo ilikuwa na Kazi Kubwa ya changamoto lakini hawakuchoka kufikia hatua hiyo ya kukamilisha utaratibu wa mwisho wa kujiunga na EAC.

Alisema Jumuiya hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa Somalia na nchi zote wanachama kwa kuwa nchi ya nane kujiunga na Jumuiya hii na tunaleta mchango Mkubwa tutakaotoa kuleta maendeleo ndani ya nchi zetu katika uchumi biashara n.k.

Ameeleza kwamba changamoto zipo ndani ya Somalia tunaendelea kuzifanyiakazi na Kwa mwaka uliopita Kuna mambo mengi tulioyafanya kuhakikisha tunawapa Picha nzuri wanachama wengine kukiwa na wanachama zaidi ya 350.


Awali Waziri wa viwanda na biashara wa Somalia,Jibril Abdirashid Haji Abdi amesema wanaendelea na wanayofuraha kuwa sehemu ya nchi nane za Jumuiya hiyo ya EAC na wanashukuru kwa kukaribishwa Rasmi na kuahidi kushirikiana na nchi zengine za Jumuiya hiyo kukuza uchumi. 


Mwisho.

DKT. MPANGO TUSIKATE MITI HOVYO”-

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Na Anangisye Mwateba-Tanga

Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Phillip Mpango amewataka wananchi kutokata miti hovyo ili kulinda mazingira na uoto wa asili uliopo sasa.

Dkt. Mpango ameyasema hayo leo Februari 21,2024 katika kijiji cha Kabuku wilayani Handeni ikiwa ni siku ya kwanza ya Ziara yake ya Siku tatu mkoani Tanga.

Mhe. Dkt. Mpango amewataka wananchi kupanda miti kwa wingi ili kuhifadhi mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabia Nchi ambayo kwa sasa yamepelekea kuwa na joto kali hasa kwa ukanda wa Pwani.

Vilevile, Mhe. Dkt Mpango alisisitiza jukumu la kutunza uoto wa asili ni la kila mtanzania hivyo ni vema kushiriki katika utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti kwa wingi.

Awali akitolea ufafanuzi wa baadhi ya changamoto zilizotolewa na Mbunge wa Handeni Mjini Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula(Mb) alimhakikishia Makamu wa Rais kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki(Mb) kuwa watazilinda maliasili za nchi hii kwa weledi na wivu mkubwa.

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa wizara ya Maliasili na Utalii imefanya vikao na wabunge wa nchi nzima ikiwemo mkoa wa Tanga ili kusikiliza changamoto, ushauri na mapendekezo yao kuhusiana na sekta za wanyamapori, misitu, utalii na malikale.


Aidha,Mhe. Kitandula alisema kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii inatarajia kufungua Geti jipya la Kuingilia hifadhi ya Taifa ya  Saadani kupitia eneo la kwa Msisi Wilaya ya Handeni mwaka ujao fedha 2024/2025.

RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN APOKEA TAARIFA YA MAANDALIZI YA MAZISHI

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Kikao cha kupokea Taarifa ya Maandalizi ya Mazishi ya Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Lowassa tarehe 16 Februari, 2024. Kikao hicho kimefanyika Ikulu Ndogo ya Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo  Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.  John Mongella.






MCHANGO WA LOWASSA KATIKA KITUO CHA KIMATAIFA CHA MIKUTANO CHA ARUSHA (AICC)

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Mwamba wa Kaskazini Hayati Edward Lowassa akiwa katika Mkutano wa Utalii wa Mikutano Jijini Rio de Janeiro Nchini Brazil Mwaka 1989.Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Masoko na Mikutano wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Danford Mpumilwa.

Je Mwamba Lowassa ana mchango gani katika Utalii wa Mikutano akiwa AICC) ? Lakini pia michezo katika jiji la Arusha na katika Klabu ya Waandishi wa Habari Arusha(APC) . Makala kamili Kesho asubuhi

EDWARD LOWASSA NI MWAMBA WA KASKAZINI

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Na Novatus Makunga.

Leo Ijumaa ya tarehe 16 Februari 2024 ndiyo siku rasmi ya kutoa heshima ya mwisho kwa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa kijijini kwake Ngarash wilayani Monduli Mkoani Arusha.

Ni nafasi pekee kwa wananchi wanaoishi mikoa ya kanda ya kaskazini ambayo ni pamoja na Arusha, Manyara na Kilimanjaro.

Nianze kwa kueleza kuwa mwanzoni baada ya kutangazwa kwa msiba huo mkubwa nchini katika andiko la kwanza kabisa nilitu.


mia Mwamba wa Kaskazini lakini wadau wakanikosoa na kuja na hoja kwamba Mzee hakuwa Mwamba wa kaskazini bali Ni Mwamba wa Tanzania na wengine wakaenda mbali kuwa ni Mwamba wa Afrika ya Mashariki. Wote walikuwa na hoja zenye mashiko hivyo nawakubaliana nao Mzee Edward Lowassa ni MWAMBA. 

Mwamba, kwangu mimi kwa mara ya kwanza nilibahatika kufahamiana naye mwaka 1993. Nilikutana naye katika kazi nikiwa Mwandishi wa habari mchanga mno.

Mwamba wakati huo alikuwa Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na alikuwa katika ziara ya kikazi mkoani Kilimanjaro.

Nilivutiwa sana na uwezo wa akili yake katika kuchanganua mambo.

Mwenyeji wake alikuwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro(RC) wa wakati huo Marehemu Samuel Sitta. Tulitoka Arusha na kaka yangu katika tasnia Noel Thomas, yeye akiwa mzoefu. 

Ilikuwa bonge ya ziara kwani kazi ilikuwa ngumu lakini habari kwa maana 'story' za kuipasha jamii zilipatikana, lakini kikubwa tulikuwa na viongozi makomredi katika siasa na wapambanahi ambao kwa wakati huo walikuwa 'moto wa kuotea mbali* 


MWAMBA LOWASSA ZAIDI YA UNAVYOMFAHAMU

1.Mwamba kwa  siasa za Tanzania alikuwa ni mwanasiasa bora wa wakati wote 'All Seasons Politician'.Ni Mtu bingwa sana wa siasa za kimikakati ambaye alikuwa tishio kwa washindani wake kisiasa. Alikuwa mtaalamu katika  siasa za Majukwaani. Mwamba alijua aseme nini na wapi kulingana na hadhira.Mwamba alikuwa mwanasiasa aliyehakikisha hatengenezi mahasimu wa kisiasa bali alijitahidi hata  maadui zake kisiasa kuwa marafiki 

2. Ni vigumu mno kumsahau mtu. 

Mwamba alikuwa na sifa moja kubwa ya kutomsahau mtu kwa sura na jina. Ilikuwa ni ajabu katika ziara iwe Kilimanjaro, Arusha, Shinyanga au Mtwara ama kona yoyote ya nchi katika ziara zake.Mwamba alikuwa anawatambua kwa majina mpaka maofisa tarafa au wenyeviti wa vijiji.

3. Kuwajali na kuwathamini anaofanyanao kazi. 

Mwamba alikuwa na tabia ya kuhakikisha anaofanya nao kazi wapo kwenye 'Comfort Zone'. Ni marufuku kuwa na kero zisizo na msingi, mfano kwa waandishi wa habari. Mwamba katika ziara zake alikuwa yupo radhi tukutane naye hata saa sita usiku kwa ajili ya tathimini ya ziara na siku ya pili ziara ikaendelea kwa kuanza kwa muda uliopanga mapema alfajiri. 

4.Chanzo Kikubwa cha habari

Kwa Mwandishi wa habari yeyote kupata habari nzito ambayo itayopendwa na jamii ndiyo kipaumbele na hapo Mwanahabari anakuwa salama. Mwamba alikuwa na sifa kubwa ya kuwa chanzo cha 'story' kubwa sana na ambazo zinatikisa. Kwa msingj huo alikuwa kiongozi pekee wa kisiasa nchini aliyekuwa karibu sana na rafiki mkubwa wa Wanahabari. 

5. Mtu wa Hoja zaidi kuliko nguvu. 

Mwamba Kama mwanasiasa alikuwa mtu wa mikakati ambaye alihakikisha kila hoja kinzani inapata majibu sahihi kwa muda muafaka. Waandishi wa habari tulikuwa tunafahamu ukitaka kuvuka "Yellow Ribbon" yake jiandaye kubishania hoja ukimshinda anakuwa mpole lakini atakupa mtazamo wake. Ni kiongozi pekee wa ngazi yake ambaye  unaweza kumpata kwa njia ya simu kwa muda wowote. Hii ina maana anapokea simu tofauti na viongozi wengi. 

ASANTE MWANBA LOWASSA, PUMZIKA KWA AMANI

BILIONI 1.6 KULIPA KIFUTA JASHO/ MACHOZI

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Na. Anangisye Mwateba-Dodoma

Wizara ya Maliasili na Utalii imekamilisha mchakato wa kufanya tathmini ya malipo ya kifuta jasho/ machozi ambapo kiasi cha shilingi Bilioni Moja na Milioni Mia Sita zinatakiwa kulipwa kupitia Wizara ya Fedha.

Haya yamebainika wakati Naibu waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula akijibu swali la Mhe. Dkt. David Mathayo David(Mb) aliyetaka kujua lini Serikali itafanya mapitio ya Sheria na Kanuni za fidia kwa waathirika wa wanyamapori ili kulipa fidia ya gharama halisi tofauti na sasa.

Aidha, Wizara imekamilisha mapitio ya Kanuni za Kifuta Jasho/Machozi na kuiwasilisha Wizara ya Fedha ili kuona uwezekano wa kuongeza viwango hivyo.

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa kwa sasa Wizara ya Fedha inafanya tathmini ili kuona athari za kiuchumi na uwezo wa nchi kutekeleza suala hilo.

"Wizara imekuwa ikilipa kifuta jasho/ machozi kama mkono wa pole au faraja kwa wananchi wanaopata madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu. Malipo hayo yamekuwa yakifanyika kwa mujibu wa Kanuni za Kifuta Jasho/Machozi za mwaka 2011 na kwa kadri ya upatikanaji wa fedha" alisema Mhe. Kitandula.

Pia, Mhe. Kitandula aliongeza kuwa wizara inafahamu kumekuwa na changamoto ya ucheleweshaji wa malipo hayo,  sababu kubwa ikiwa ni ulazima wa kufanyika kwa tathimini ya kina inayolazimu kwenda uwandani ili kuhakiki na kujiridhisha kiwango cha uharibifu au madhara yaliyojitokeza na fidia stahiki inayopaswa kutolewa.

VIWANDA 7 VYA KUCHAKATA MAZAO YA ASALI VYAJENGWA

HOJA NEWS BLOG Add Comment

Na. Anangisye Mwateba- Dodoma

Serikali imewezesha ujenzi wa viwanda saba (7) vya kuchakata na kufungasha asali katika Wilaya za Sikonge, Mlele, Nzega, Tabora, Manyoni, Kibondo na Bukombe vitakavyotumika kuongezea thamani asali inayozalishwa na kuuzwa katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Haya yamebainika wakati Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula(Mb) akijibu swali la Mhe. Athuman Almas Maige Mbuge wa Tabora Kaskazini katika kikao cha cha tatu cha Mkutano wa 14 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaondelea jijini Dodoma aliyetaka kujua Je Serikali ina mpango gani wa kufanya asali kuwa moja ya zao la kimkakati?

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa ufugaji nyuki ni moja ya shughuli muhimu za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa makabila mengi hapa nchini, Afrika na katika maeneo mengi duniani. 

Aidha, ufugaji nyuki una mchango mkubwa katika kuhakikisha usalama wa chakula kupitia uchavushaji. Ufugaji Nyuki ni miongoni mwa shughuli za kiuchumi hasa kwa jamii inayoishi kando kando na maeneo yaliyohifadhiwa.

‘Kwa kutambua umuhimu wa shughuli hii, Serikali imechukua hatua kadhaa za kufanya asali kuwa zao la kimkakati. Hatua hizo ni pamoja na: Kuimarisha mifumo ya usimamizi pamoja na kutunga na kutoa miongozo mbalimbali inayohusu ufugaji nyuki; kuwezesha wafugaji nyuki kwa kuwapatia mizinga ya kisasa. Mathalan katika kipindi cha miaka mitano (5) iliyopita zaidi ya mizinga ya kisasa 64,593 imetolewa kwa vikundi vya wafugaji nyuki kutoka katika mikoa mbalimbali”. Mhe. Kitandula alisema

Mhe. Kitandula aliongeza kuwa  Serikali inatekeleza programu na miradi mbalimbali ya kuwezesha kuongeza uzalishaji wa asali sambamba na kutafuta masoko mapya ya asali katika nchi za Umoja wa Ulaya na Asia. 

Pia aliongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo inatekeleza mradi wa kuwezesha ufugaji nyuki katika mikoa mitano (Tabora, Singida, Katavi, Kigoma na Shinyanga) kwa upande wa Tanzania Bara na Kisiwa cha Pemba kwa upande wa Zanzibar. 

Vilevile, Serikali inakamilisha Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Ufugaji Nyuki ambao utachochea uzalishaji, mauzo ya asali nje ya nchi pamoja na ajira hasa kwa vijana na wanawake.

Mwisho